Posts

Pre-energy, Neotonic Ni Tiba Kwa Ajili Ya Kiwango Kikubwa Cha Lehemu (High Cholestrol)

Image
Ugonjwa wa moyo na mishipa, ndio sababu kuu ya vifo ulimwenguni pote, unaweza kuletwa na lehemu (cholesterol) nyingi. Kama matokeo, unapaswa kutengeneza kiwango cha lehemu kwa ajili ya afya yako. Neotonic ina mchanganyiko wa viambata vya mbogamboga aina 6 na matunda aina 2, na Pre-energy ina mchanganyiko wa viambata vya mbogamboga aina 3 na matunda aina 2. Kulingana na utafiti , viambata vya Pre-energy na Neotonic ambapo mojawapo ni tangawizi ambayo inapokuwa kwenye mchanganyiko wa viambata vingine ni tiba bora ya kiwango kikubwa cha lehemu au mafuta kwenye damu (high cholesterol ).  Kutokana na hali hiyo, watu wengi tunawahimiza kutumia tiba nzuri za asili kutoka James Herbal Clinic. Kila kitu unachohitaji kujua kuhusu vipengele vya dawa hi z i na uwezo wake wa kuimarisha afya yako, kama inavyoungwa mkono na watu wengi waliotumia wakaona faida yake kubwa, basi unaweza kufika kituoni kwetu au ukawasiliana nasi kwa namba zilizotajwa hapo chini. Mambo Unayopaswa Kujua Kuhusu Kiwango ...

Haya Ndio Mambo 4 Unayoweza Kuyakosea Katika Kutambua Maambukizi Ya Fangasi

Image
Maambukiz haya yenye kuchukiza hutokea kwasababu ya kukua kwa bakteria aina ya Candida albicans, na ni wa kawaida kabisa, kwani huathiri wanawake 3 katika wanawake 4 katika maisha yao. Japokuwa maambukizi ya fangasi yanazidi kuongezeka kwa kasi, basi unapoona dalili kama vile muwasho mkubwa, ukiambatana na uchafu mwingi mweupe pamoja na hali ya kuwaka moto, basi usichelewe kimbia haraka maabara au hospitali ukapate vipimo. Lakini yapo maambukizi mengine yanayofanana na ugonjwa huu na yanayweza kusababisha dalili zenye kufanana na fangasi, lakini matibabu yake ni tofauti. Leo napenda nikuonyeshe baadhi ya maambukizi haya ili uyafahamu vizuri. Karibu katika makala yetu. 1.  Kisonono Na Pangusa Maambukizi ya fangasi yana tabia ya kuzarisha uvimbe, na ndio maana unaona dalili hizo. Kitu chcochote kinachoweza kuonekana kama uvimbe kinaweza kusababisha uvimbe. Magonjwa ya maambukizi ya zinaa kama vile pangusa na kisonono yanaweza kusababisha hali hiyo. NUKUU: Uchafu wa fangasi sehemu za ...

Je Mitume walitunza Sabato Jumamosi? Sehemu ya 2

Image
Baada ya Paulo na Barnaba kushindana, Barnaba alienda pamoja na Yohana, wakati Paulo alienda pamoja na Sila (Mdo 15:37-40). Paulo na Sila wakapitia Shamu na Kilikia, Derbe na Listra ambapo walimpitia Timotheo, kisha wakasafiri kwenda nchi ya Frigia na Galatia, wakapitia Misia, na Bithinia, na Troa ambapo Paulo alipata maono akiambiwa avuke kwenda Makedonia, na kutoka hapo wakasafiri hadi Samothrake na Neapoli; na kutoka hapo wakafika Filipi mji mkuu wa jimbo la Makedonia.   Matendo 16:12 “na kutoka hapo tukafika Filipi, mji wa Makedonia, mji ulio mkuu katika jimbo lile, mahali walipohamia Warumi; tukawa katika mji huu, tukikaa siku kadha wa kadha.”   Paulo akiwa na Sila na Timotheo pamoja na Luka mwenyewe ambaye ni mwandishi wa kitabu cha Matendo, walipofika Filipi walikaa hapo siku kadhaa. Je Paulo alitunza Sabato huko Filipi au alitunza Jumapili? Angalia Luka mwenyewe ambaye alikuwa pamoja na Paulo huko Filipi jinsi anavyoshuhudia:   Matendo 16:13 “Hata siku ya sabato t...

Je Jumapili ni Sabato ya Wakristo?

Image
Katika ukurasa huu natumaini kushiriki nawe baadhi ya mafungu ya Biblia ambayo yamechukuliwa nje na maana zake halisi ili kuonyesha kuwa Jumapili ni Sabato ya Kikristo. Mkristo wa kweli siku zote hataamini mawazo tu ya viongozi wa kanisa lake, lazima atafute kujua ukweli yeye mwenyewe kwa kufuatilia kama viongozi wake wako katika kweli au uongo. Fikiria kuhusu hili kwa muda, umeweka tumaini lako kwa kiongozi wako wa kanisa kana kwamba yeye hawezi kukosea, na kila anachokufundisha unaamini asilimia 100% na hautaki kuchunguza mwenyewe. Uko katika hatari kubwa! Kama shetani akimuongoza huyo kiongozi wako katika njia ya upotofu, ataangusha kanisa zima la wale wanaomwangalia kiongozi huyo na kumwamini 100%. Na hiki ndicho kifaa cha shetani ambacho amefanikiwa kuweka watu katika mtego wake; kwa sababu anajua Wakristo wengi duniani wanawaangalia viongozi wao kana kwamba hawawezi kukosea katika kuhubiri ukweli wa Biblia, hivyo, juhudi zote za shetani ni kuwawinda viongozi awashike katika mtego...

Je, Mitume walitunza Sabato Jumamosi?

Image
Imedaiwa miongoni mwa wajumapili kwamba Yesu alipofufuka siku ya Jumapili, na Roho Mtakatifu aliposhuka siku ya Jumapili katika Pentekoste, kwa kitendo hicho Yesu aliitakasa jumapili ili watu wake badala ya kutunza Jumamosi waanze kutunza Jumapili.  Lakini kama ukirudi katika Maandiko na kuangalia kwa makini, hautaona mahali popote ambapo Yesu Mwenyewe au mtakatifu yeyote amesema kwamba Jumapili ilitakaswa na kubarikiwa. Nataka kuvuta usikivu wako tuchunguze kwa makini katika Biblia ili tuone ni siku gani ambayo Yesu alitakasa. Na Je Yesu alitakasa Jumapili? Ushahidi katika vitabu vya Injili Katika Agano Jipya siku ya kwanza ya juma imetajwa mara 8 tu, na mara zote haijasemwa popote kwamba imetakaswa au kwamba Mungu aliagiza watu watunze siku hiyo.   Katika Kitabu cha Mathayo siku ya kwanza ya juma imetajwa mara moja ikihusiana na ufufuo wa Yesu,  na hakuna ibada iliyofanyika siku hiyo, bali Sabato ilipoisha ndipo Mariamu siku ya jumapili alienda kaburini na akakuta Yesu ...