Fahamu Madhara Yanayotokana Na Ugonjwa Wa PID Wa Muda Mrefu

Ugonjwa wa PID usipopata tiba yake unaweza kusababisha matatizo makubwa ya muda mrefu kwa mgonjwa. Matatizo haya huwa kama ifuatavyo:

  • Ugumba: Mwanamke mmoja kati ya 10 wenye PID hushindwa kuwa na uwezo wa kupata mimba na hivyo kuwa mgumba. PID inaweza kusababisha makovu kwenye mirija ya uzazi. Makovu haya yanaweza kuiziba mirija na kuzuia yai kushindwa kurutubishwa.
  • Mimba Kutunga Nje Ya Uzazi: Kovu kutokana na PID pia linaweza kuzuia yai lililorutubishwa kushindwa kutoka kwenye mrija wa uzazi na kuhamia kwenye mfuko wa uzazi. Badala yake, linaweza kuanza kukua huku likiwa ndani ya mrija wa uzazi. Mrija unaweza kupasuka na kusababisha damu inayohatarisha maisha ndani ya tumbo la uzazi na kwenye nyonga. Upasuaji wa dharura unaweza kuhitajika ikiwa mimba nje ya tumbo la uzazi haitatambuliwa mapema.
  •  Maumivu Ya Nyonga Ya Muda Mrefu: PID inaweza kusababisha maumivu ya nyonga ya muda mrefu ambayo hudumu Zaidi ya miezi 6.

Je, Nani Yuko Kwenye Hatari Ya Ugonjwa Wa PID?

PID inaweza kutokea katika umri wowote kwa wanawake wanaofanya ngono. Ni kawaida zaidi Kwa wanawake wenye umri mdogo. Narudia tena, wale walio chini ya umri wa miaka 25 wana uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa wa PID. Wanawake walio na sababu zifuatazo za hatari pia wana uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa wa PID, kama vile:

  • Maambukizi ya zinaa kama vile kisonono na pangusa
  • Kuwa na wapenzi wengi
  • Kuwa na mpenzi mwenye wapenzi wengi
  • Uliwahi kuwa na PID ikapona tena ikarudia, nk.

Utafiti fulani unaonyesha kuwa wanawake wanaoosha sehemu zao za uke kwa kutumia sabuni zenye marashi makali, wapo kwenye hatari kubwa ya kupata PID. Kutawaza ukeni kwa kuweka vitu vyenye marashi knaweza kurahisisha bakteria wanaosababisha PID kukua. Pia inaweza kuwafanya bakteria kutoka ukeni na kuhamia kwenye tumbo la uzazi, na kwenye mirija ya uzazi. Kwa namna hiyo basi, kutawaza uke kwa kuosha na vitu vyenye marashi makali, hakufai. 

Je, Ugonjwa Wa PID Unaweza Kuuziaje?

Ili kusaidia kuzuia ugonjwa wa PID, chukua hatua zifuatazo ili kuepuka magonjwa ya zinaa:

  •   Kuwa na mpenzi mmoja unayemwamini na wote muwe waaminifu
  • Shiriki mapenzi na mpenzi ambaye hajawahi kuwa na magonjwa ya zinaa na awe mpenzi wako mwenyewe tu,
  • Punguza idadi ya wapenzi na ikiwezekana, achana na wapenzi wengine, halafu uwe na mpenzi mmoja tu.
  • Epuka kutoa mimba kabisa
  • Jitahidi kuwa na mwenza wako kama mume au mke wako ili muishi kwa pamoja kwa kuaminiana. 

Je, Nini Kifanyike Ili Kuondoa Ugonjwa Wa PID?

James Herbal Clinic tunazo dawa nzuri kabisa zenye uwezo mkubwa wa kutatua tatizo hili na madhara yake, nazo ni MULTICURE POWDER, PERFECT POWDER na CARD HERB. 

Asante sana msomaji, makala yetu inaishia hapa, nikaribishe kipindi cha maswali na maoni yako.
Pia unaweza kutuma namba yako ya WhatsAp tukakuunganisha na darasa letu ili uweze kujifunza zaidi masomo ya afya.

Unahitaji Huduma? Basi, wasiliana nasi kupitia namba hizi: 0768 559 670 au 0712 181 626,

Arusha-Mbauda,

Karibu sana!




 



Comments

Popular posts from this blog

Fahamu Mambo Yanayosababisha Uke Kulegea

Aina 9 Ya Vyakula Unavyopaswa Kuviepuka Unapokuwa Na Tatizo La Figo

Mambo 6 Yanayopelekea Mwanamke Kuhisi Maumivu Makali Anaposhiriki Tendo La Ndoa