Fahamu Mambo Yanayosababisha Uke Kulegea

Misuli ya nyonga huzunguka uke. Misuli hii inaweza kudhoofika kwa muda, hali ambayo inaweza kusababisha hisia ya uke kulegea.

Baada ya kujifungua au kadiri mtu anapokua na umri mkubwa, misuli inayozunguka uke inaweza kudhoofika. Hata hivyo, hali hii huwa haidumu daima kwa sababu misuli ya uke inayotanuka inaweza kutanuka na kurudi kwenye umbo lake la kawaida.

Misuli inayozunguka uke inapodhoofika inaweza kusababisha matatizo kama vile kutoweza kujizuia, na kusababisha mkojo kutoka wenyewe. Mazoezi ya misuli kwenye nyonga yanaweza kusaidia kuimarisha misuli ya uke.

Wakati Wa Kushiriki Tendo La Ndoa

Wakati mwili unapopata hamu au nyege, uke huwa na unyevunyevu, na misuli yake hulegea, ambayo huwezesha uume kupita kwa urahisi.

Walakini, misuli hii hulegea polepole, ndiyo maana nyege inaweza kuwa ya muhimu sana kabla hujaanza kushiriki tendo la ndoa. Baada ya tendo la ndoa, uke huwa unarudi kwenye umbo lake la kawaida na kuvutika kama mpira.


Uke huwa wazi zaidi kwa muda kabla ya tendo la ndoa, au wakati wa tendo la ndoa au baada ya ya tendo la ndoa. Hali hii ni sawa na mdomo unapotanuka wakati unapokula kula au unapopiga miaye, halafu unarudi katika umbo lake la kawaida.

Ubikira ni utando mwembamba unaozunguka uke. Unapofanya tendo la ndoa na mara ya kwanza na uume ukapita, unaweza kutanua bikira kidogo, hali ambayo inaweza kuufanya uke wazi kidogo.

Hakuna miili miwili inayofanana, na unapofanya tendo la ndoa na mwenzi mpya unaweza kuhisi tofauti sana. Miili pia hubadilika kulingana na umri, kukonda au kunenepa sana. Pamoja na ugonjwa.

Kujaribu mkao au style  tofauti ya tendo la ndoa wakati mwingine kunaweza kubadilisha jinsi uke unavyohisi kubana au kulegea. Hii inaweza kuboresha raha ya tendo la ndoa kwa wenzi wote wawili.

 Wakati Wa Kujifungua

Mwili hupitia mabadiliko mengi wakati wa ujauzito na baada ya kujifungua. Mabadiliko haya yanaweza kuwa pamoja na:

  • kuvimba miguuni
  • mwili kukonda au kunenepa
  • badiliko kwenye matiti, ukubwa au umbo lake
  • alama ya michirizi kwenye ngozi
  • miguu kuwa mikubwa, nk

Wakati wa kujifungua, mtoto anapopita ukeni, misuli ya uke hutanuka. Umbo hili la kutanuka hupungua taratibu. Baada ya kujifungua, misuli ya uke haiwezi kuwa kama ilivyokuwa mwanzo, na inaweza kuchukua muda kurekebika na kuwa katika hali ya mwanzo.

Baadhi ya wanawake hupeleka taarifa za  mabadiliko katika umbo la uke au unyumbufu baada ya kujifungua. Wakati mwingine, mwanamke anaweza kuhisi hisia kidogo au kutosheka wakati wa tendo la ndoa, lakini hisia hizi kawaida hurudi kwa wakati.

Uharibifu wa ngozi, tishu, au misuli wakati wa kujifungua  pia unaweza kusababisha mabadiliko kwenye mashavu ya uke na kwenye uke. Hii inaweza kuleta tofauti katika jinsi uke unavyolegea au kubana.

Wakati Umri Unapozidi Kuongezeka

Mwili hubadilika kadiri unavyozeeka. Ngozi na misuli hudhoofika taratibu, hali ambayo husaidia kueleza kwa nini uke unaweza kuanza kujisikia kulegea. Wakati wa kukoma hedhi, viwango vya homoni ya estrojeni hupungua. Hali hii inaweza kusababisha utando wa uke kuwa mkavu na kutanuka kidogo sana.

Uke unaweza kuwa mfinyu au mfupi baada ya kukoma hedhi. Pia, kunaweza kuwa na usumbufu, hususani unaosababishwa na kupungua kwa uteute, wakati wa kushiriki tendo la ndoa. Kufanya mapenzi mara kwa mara wakati wa kukoma hedhi kunaweza kusaidia kuzifanya tishu za kwenye uke kuwa nene.

Wakati unapokaribia kukoma hedhi au unapokoma hedhi, ni ukuta wa uke kubadirika. Pia, tendo la ndoa unaweza kurihisi tofauti, na uke unaweza kuwa mkavu. Kwahiyo ni jambo la kawaida kabisa maana muda tayari umefika mwisho, huhitaji kuzaa tena.

MUHIMU: Uke unaobana huleta raha kubwa mno kwa wote wawili wakati mnaposhiriki tendo la ndoa. Uke uliolegea au kupanuka huwaondolea raha wote wawili.

Makala yetu inaishia hapa, nakaribisha kipindi cha maswali na maoni yako.

Je, Suluhisho Ni Nini?

James Herbal Clinic tunazo dawa nzuri zenye uwezo mkubwa wa kurudisha uteute na pia kuufanya uke kuwa katika hali yake ya mwanzo. Unaweza kutuma namba yako ya WhatsAp ili tuweze kukuunganisha na darasa letu la masomo ya afya.

Unahitaji huduma, basi wasiliana nasi kwa namba hizi: 0768 559 670/0712 181 626,

Arusha-Mbauda,

Karibu sana!


Comments

Popular posts from this blog

Aina 9 Ya Vyakula Unavyopaswa Kuviepuka Unapokuwa Na Tatizo La Figo

Mambo 6 Yanayopelekea Mwanamke Kuhisi Maumivu Makali Anaposhiriki Tendo La Ndoa