Fahamu Mambo 3 Yanayopelekea Kuvimba Kwa Shingo Ya Kizazi
Kuvimba kwa shingo ya kizazi kitaalamu tunaita, “Cervicitis”, nayo huwa ni sehemu nyembembe inayokuwa chini mwishoni mwa tumbo la uzazi ambayo hufunguka ndani kwenye uke.
Dalili za
kuvimba kwa shingo ya kizazi ni pamoja na kutokwa na damu ya hedhi kwa
kujirudia mara mbili ndani ya mwezi mmoja, kuhisi maumivu wakati unaposhiriki
tendo la ndoa, na kutokwa na uchafu ukeni. Hata hivyo, pia inawezekana kupatwa
na hali ya kuvimba kwa shingo ya kizazi na kushindwa kuona dalili au ishara
zozote.
Mara nyingi, kuvimba kwa shingo ya kizazi kunaweza kutokana na maambukizi ya magonjwa ya zinaa, kama vile pangusa au kisonono. Uvimbe wa shingo ya kizazi unaweza kutokana na magonjwa ya siyo ambukiza pia. Matibabu ya ugonjwa huu huhusika na kutiba uvimbe wa shingo ya kizazi.
Mara nyingi, kuvimba kwa shingo ya kizazi huwa hauonyeshi dalili, na unaweza kujifunza tu ugonjwa baada ya kupata vipimo. Ikiwa kama una dalili, basi zinaweza kuwa pamoja na hizi zifuatazo:
- Kutokwa na uchafu mwingi usio wa kawaida ukeni
- Kuhisi maumivu wakati unapokojoa mara kwa mara
- Kuhisi maumivu wakati unaposhiriki tendo la ndoa
- Kutokwa na damu ya hedhi kujirudia mara mbili ndani ya mwezi mmoja
- Kutokwa na damu ukeni baada ya kumaliza kushiriki tendo la ndoa
Je, Nini Visababishi Vyake?
Visababishi
vinavyofanya shingo ya kizazi kuvimba ni hivi vifuatavyo:
1. Maambukizi Ya Magonjwa Ya Zinaa
Mara nyingi,
maambukizi ya bakteria au virusi ambayo husababisha shingo ya kizazi kuvimba
huambukizwa kupitia ngono. Kuvimba kwa shingo ya kziazi hutokana na maambukizi
ya zinaa, ikiwa pamoja na kisonono, pangusa, malengelenge pamoja na mkanda wa
jeshi.
2. Athari Za Mzio
Mzio, au dawa za
uzazi wa mpango au kondom, vinaweza kupelekea shingo ya kizazi kuvimba. Athari
za bidhaa za wanawake kwa ajili ya usafi, kama vile sabuni zenye kuondoa
harufu, pia zinaweza kusababisha kuvimba kwa shingo ya kizazi.
3. Bakteria Kukua Kwa Kasi
Bakteria wanaokua na kuzaliana kwa wingi ukeni kwa kawaida hupelekea shingo ya kizazi kuvimba.
Je, Nini
Vihatarishi?
Uko katika
vihatarishi vikubwa vya kuvimba kwa shingo ya kizazi, ikiwa kama:
·
Una
tabia ya kushiriki tendo la ndoa bila kinga, kuwa na wapenzi wengi au kushiriki
tendo la ndoa na mtu ambaye ana tabia ya kushiriki na wapenzi wengi
·
Ulianza
kushiriki tendo la ndoa mapema ukiwa bado mdogo
· Uliwahi kupatwa na magonjwa ya zinaa.
Je, Nini Madhara Ya Kuvimba Kwa Shingo
Ya Kizazi?
Shingo yako ya
kizazi hufanya kazi kama kinga ili kuzuia bakteria na virusi wasiweze kuingia
kwenye tumbo la uzazi. Wakati shingo ya kizazi inapoambukizwa, kuna vihatarishi
vikubwa kwamba maambukizi watasafiri na kuingia kwenye tumbo la uzazi.
Uvimbe wa shingo
ya kizazi ambao husababishwa na kisonono au pangusa unaweza kuenea kwenye ukuta
wa tumbo la uzazi na kwenye mirija ya uzazi, na hivyo kusababisha PID, maambukizi kwenye viungo vya uzazi
vya mwanamke ambayo yanaweza kusababisha matatizo ya uzazi ikiwa kama hayajatibiwa.
Kuvimba kwa
shingo ya kizazi pia kunaweza kuongeza vihatarishi vya kupata HIV kutoka kwa
mpenzi mwenye maambukizi.
Je, Suluhisho Lake Ni Nini?
James Herbal
Clinic tunazo dawa nzuri kabisa zenye uwezo mkubwa wa kuondoa vyanzo vya
kuvimba kwa shingo ya kizazi, nazo ni MULTICURE
POWDER, PERFECT POWDER na CARD HERB.
Ndugu msomaji, Makala
yetu ndio inaishia hapa, nikaribishe kipindi cha maswali na maoni yako. Pia
unaweza kutuma namba yako ya WhatsAp ili tuweze kukuunganisha na darasa letu la
masomo ya afya.
Je, Unahitaji
Huduma? Basi wasiliana nasi kwa namba hizi: 0768 559 570 au 0712 181 620,
Arusha-Mbauda.
Karibu sana!
Comments
Post a Comment