Fahamu Sababu Zinazomfanya Mwanamke Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa?

Viwango vya wanawake vya hamu ya tendo la ndoa hupungua kadiri wanavyozidi kukua. Ni kawaida viwango vya juu na vya chini kutokea pamoja katika mwanzo au mwisho wa mahusiano. Au viwango hivi vinaweza kutokea kwa mabadiliko makubwa ya maisha kama vile ujauzito, kukoma hedhi au ugonjwa. Dawa zingine zinazotumiwa kwa ajili ya kutibu magonjwa fulani zinazoathiri hisia pia zinaweza kusababisha kushuka kwa hamu ya tedno la ndoa kwa mwanamke.

Ikiwa kama hali ya kukosa hamu ya tendo la ndoa inaendelea au inatoweka tena inarudia, na kusababisha shida zako kibinafsi, basi ongea na mtaalamu wako wa afya. Unaweza kuwa na ugonjwa unaoweza kutibika unaoitwa ugonjwa wa kukosa hamu au hisia ya tendo la ndoa.

Je, Dalili Zake Ni Nini?

Na hata kama hamu yako ya tendo la ndoa iko chini sana kuliko ilivyokuwa hapo awali, bado uhusiano wako unaweza kuwa na nguvu. Nipende kuema hivi: Hakuna kiwango kinachoweza kufafanua upungufu wa hisia au hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke. Ni hali inayotofautiana.

Dalili za kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake ni pamoja na:

  • Kufurahia kidogo au kutokufurahia kabisa aina yoyote ya shughuli za ngono, ikiwa ni pamoja na kupiga punyeto.
  •  Ni mara chache tu unaweza kuwa na hamu ya tendo la ndoa au kukosa kabisa.
  • Kuwa na huzuni au mawazo sana kutokana na kukosa hamu ya tendo la ndoa,

Je, Vyanzo Vyake Ni Nini?

Hamu ya tendo la ndoa inategemeana na mchanganyiko wa mambo mengi yanayoathiri urafiki wako na mwenza wako. Sababu hizi ni pamoja na:

  • Ustawi wa kimwili na kihisia.
  • Uzoefu
  • Imani
  • Uhusiano wako sasa
  • Mitindo ya maisha,

Ikiwa una changamoto katika mojawapo ya maeneo haya, inaweza kuathiri uwezo wa hamu yako ya tendo la ndoa.

Sababu Za Kimwili

Magonjwa mbalimbali, mabadiliko ya mwili pamoja na madawa vinaweza kusababisha hisia au hamu ya tendo la ndoa kuwa kidogo, ikiwa, pamoja na:

  • Matatizo Ya Uzazi: Ikiwa unapata maumivu wakati wa kushiriki tendo la ndoa, au huwezi kufika kileleni, inaweza kupunguza hisia au hamu yako ya tendo la ndoa.
  •  Magonjwa: Magonjwa mengi yasiyo ya uzazi yanaweza kuathiri hamu ya tendo la ndoa. Haya ni pamoja na saratani, kisukari, shinikizo la damu, ugonjwa wa mishipa ya moyo na magonjwa ya mishipa ya fahamu.
  •  Tabia Ya Mitindo Ya Maisha: Glasi ya divai inaweza kukufanya ufurahi, lakini pombe nyingi zinaweza kuathiri hamu yako ya tendo la ndoa. Ndivyo ilivyo hata kwa madawa. Pia, uvutaji sigara hupunguza mtiririko wa damu, ambayo inaweza kupunguza hisia au hamu ya tendo la ndoa.
  • Uchovu Wa Mwili: Uchovu unaotokana na kubeba watoto wachanga au wazazi wanaozeeka unaweza kuchangia kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa. Uchovu kutokana na ugonjwa au upasuaji pia unaweza kuwa ni chanzo.

Mabadiliko Ya Homoni

Mabadiliko katika viwango vyako vya homoni yanaweza kubadilisha hamu yako ya tendo la ndoa. Hii inaweza kutokea wakati:

  • Kukoma Hedhi: Kiwango cha homoni ya estrojeni hupungua wakati wa kukoma hedhi. Hii inaweza kukufanya usivutiwe sana kushiriki tendo la ndoa na kusababisha uke mkavu, na kusababisha kushiriki tendo la ndoa huku unahisi maumivu makali au usumbufu. Wanawake wengi bado wanaridhisha wanaposhiriki tendo la ndoa wakati wa kukoma hedhi na baada ya hapo. Lakini wengine wanakosa hamu ya tendo la ndoa kabisa na wanashindwa kuridhisha waume zao wakati wa mabadiliko haya ya homoni.
  • Kunyonyesha Au Ujauzito: Homoni hubadirika tu wakati wa ujauzito, na baada ya kupata mtoto na wakati wa kunyonyesha inaweza kupunguza raha wakati unaposhiriki tendo la ndoa. Uchovu na mabadiliko vinaweza kubadiri umbo au sura ya mwili vinaweza kuathiri hamu ya tendo la ndoa. Vivyo hivyo ule msukumo wa ujauzito au mimba inapoingia.

Matatizo Ya Kisaikolojia 

Hali yako ya akili inaweza kuathiri hisia zako. Sababu za kisaikolojia za hisia kidogo za tendo la ndoa ni pamoja na: 

  • Matatizo ya afya ya akili kama vile wasiwasi au msongo wa mawazo
  • Msongo wa mawazo unaohusiana na mambo kama vile fedha au kazi
  • Muonekano mbaya wa mwili
  • Kutokujithamini

Masuala Ya Mahusiano

Kwa watu wengi, hisia zinapokuwa karibu, ni ufunguo wa kuwa karibu na mwenza wako. Kwa hivyo matatizo katika uhusiano wako yanaweza kuwa sababu kuu ya kukosa hisia au hamu ya tedno la ndoa. Mara nyingi, ile hali ya kutokupata raha yoyote unaposhiriki tendo la ndoa, ni matokeo ya masuala yanayoendelea kama vile:

  • Kutokuwa na mahusiano mazuri na mwenza wako
  • Migogoro au ugomvi ambao haujatulia,
  • Mawasiliano duni unapohitaji kushiriki tendo la ndoa,
  • Masuala ya uaminifu
  • Wasiwasi juu ya uwezo wa mpenzi wako kushiriki tendo la ndoa,
  • Kutokuwa na usiri wa kutosha, 

 

Je, Nini Suluhisho Lake Hasa Kwa Wanawake?

James Herbal Clinic tunazo dawa nzuri zenye uwezo mkubwa wa kuondoa vyanzo vya kukosa hisia wakati wa tendo la ndoa, nazo ni VITAMAKA, FRESH HERB na NEOTONIC.



Nipende kuishia hapa, niwakaribishe katika kipindi cha maswali na maoni yenu, karibuni sana. Pia unaweza kutuma namba yako ya WhatsAp ili tuweze kukuunganisha na darasa letu la masomo ya afya.

Je, Unahitaji Huduma? Basi, tupigie: 0768 559 670/0712 181 626,

Arusha-Mbauda,

Karibu sana!





Comments

Popular posts from this blog

Fahamu Mambo Yanayosababisha Uke Kulegea

Aina 9 Ya Vyakula Unavyopaswa Kuviepuka Unapokuwa Na Tatizo La Figo

Mambo 6 Yanayopelekea Mwanamke Kuhisi Maumivu Makali Anaposhiriki Tendo La Ndoa