Fahamu Vyakula Ambavyo Mama Hapaswi Kula Wakati Wa Ujauzito
Neno la Mungu linathibitisha kuwa watoto ni Baraka kutoka kwa Mungu. Mwanzo 1:28.
“Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha, mkatawale samaki wa baharini na ndege wa angani na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya Nchi”
Kwahiyo ili mtoto azaliwe akiwa
na afya njema pamoja na akili angavu ni lazima apate lishe bora akiwa tumboni
mwa mama yake.
Vyakula Bora Kwa Ufupi
1. Vyakula
vya nafaka na wanga –kwa ajili ya ukuaji wa mtoto.
2.
Samaki na nyama-kujenga mwili wa mtoto hasa katika miezi ya 4-9.
3.
Vyakula vya mafuta – kwa ujengaji wa seli za mwili.
4.
Mbogamboga-kuimarisha mwili na akili ya mtoto.
5. Maji- husaidia mmen’genyo na
unyonyaji wa chakula, huzuia choo kigumu, mwili kuvimba na UTI.
Makande Lishe
Ni chakula chenye mchanganyiko wanafaka zisizopungua saba pamoja na viungo mbali mbali. Mchanganyiko wake ni kama ifuatavyo: -
NAFAKA.
1.
Njugu mawe
2.
Maharage
3.
Karanga
4.
Ngano isiyokobolewa
5.
Kunde
6.
Mbaazi
7.
Dengu
8. Ufuta na mtama
VIUNGO
1.
Karoti
2.
Boga
3.
Vitunguu maji
4.
Vitunguu saumu
5. Pilipili hoho
FAIDA ZA MAKANDE LISHE
i.
Chakula cha
ubongo
ii.
Huleta kumbukumbu
nzuri
iii.
Ni lishe nzuri
kwa watoto na wazee
iv.
Ni chakula cha
ngozi, huzuia na kutibu magonjwa ya ngozi
v.
Huimarisha via
vya uzazi
Zingatia: Ukifuata kanuni na utaratibu huu, hutajifungua kwa oparesheni. Utakuwa mama mwenye afya, na utajifungua mtoto mwenye uzito mzuri na mwenye afya bora.
Kwa ushauri na huduma zingine, tutumie ujumbe au wasiliana nasi kwa namba hizi: 0768 559 670/ 0712 181 626.
Arusha-Mbauda,
Karibuni sana.
Comments
Post a Comment