Je, Unasumbuliwa Na Ugonjwa Wa UTI (Urinary Tract Infection)? Jihadhari, Unaweza Kuathiri Uzazi Wako.
Ikiwa Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) yataathiri sehemu ya juu ya mwili wako (figo, uterasi, mirija ya uzazi), inaweza kuathiri uwezo wako wa kushika mimba.
Ugonjwa wa UTI (Urinary Tract Infection) ni suala la
kawaida kwa wanawake ambalo husababishwa na kukua kwa bakteria ambao kwa ujumla
wanaitwa “E. Coli” wanaokuwa kwenye
mkojo. Wakati bakteria hao wanapozidi kuongezeka na kusogea hadi kwenye njia ya
mkojo, wanaweza kusababisha maambukizi makubwa ambayo hutambuliwa kwa dalili
kama vile homa, kichefuchefu, baridi, kutokujisikia vizuri na hali ya kuwaka
kama moto wakati unapokojoa.
Iwapo utakuwa umepata dalili za UTI, basi fika hospitali bila kuchelewa ili uweze kupata huduma ili kudhibiti maambukizi. Usipuuze dalili hizo kwani kutokujali kunaweza kusababisha matatizo ya kiafya. Mara nyingi, maambukizi mengine kama vile magonjwa ya zinaa yanaweza kuwa sababu halisi cha matatizo ya kutokupata ujauzito ambayo yanaweza kuchanganyikana na UTI kwa kuwa dalili zake zinafanana.
Suala la magonjwa ya mfumo wa mkojo huwapata wanaume na wanawake, lakini wanawake huathirika zaidi na UTI kwani njia ya mkojo ya mwanamke ni ndogo ukilinganisha na ya wanaume. Kwa hiyo, wanawake wanapaswa kuchukua tahadhari kubwa zaidi ili kuzuia UTI.
Maambukizi ya mfumo wa mkojo huathiri viungo kama vile figo, ini, mfuko wa uzazi (uterus) na kibofu cha mkojo ambacho hufanya kazi ya kutoa taka huku kikidhibiti joto la mwili. Ikiwa maambukizi yataendelea au kujirudia mara kwa mara, hasa kuathiri njia ya juu (figo, mfuko wa uzazi, mirija ya uzazi), inaweza kuathiri uwezo wako wa kushika mimba/ujauzito.
Hali hii pia huitwa ugonjwa wa maambukizi katika via vya uzazi au PID ambao unaweza kuharibu mirija ya uzazi kwa kiasi kikubwa. Madhara ya PID
Ugonjwa sugu wa figo unaweza kuathiri sehemu zingine za mwili na unaweza
kuathiri afya yako na mchakato wa upevushaji wa mayai ambao unaweza kuathiri
uwezekano wa kushika mimba.
UTI kwa wanaume pia inaweza kusababisha kushindwa
kupata ujauzito(ugumba). Maambukizi ya kwenye mfumo wa njia ya mkojo yanaweza
kusababisha utasa kwa mwanauume (kushindwa kumpa mimba mwanamke). Bakteria
huenea kwenye tezi dume na viungo vingine vya uzazi ambavyo vinaweza
kusababisha kupungua kwa idadi ya mbegu za kiume (manii) pamoja na kasi ya
kusafiri kwa mbegu.
Maambukizi yanaweza kuathiri maeneo kama vile
korodani, mirija ya kusafirisha mbegu, pamoja na tezi dume. Wakati mwingine,
hali zingine za kiafya kama vile kisukari zinaweza kusababisha UTI na
kusababisha utasa au ugumba. Walakini, shida hii inaweza kutibiwa na dawa za
asili tena kwa haraka na kwa uhakika.
Vidokezo Vya Kudhibiti UTI
James Herbal Clinic tunapendekeza tahadhari rahisi
ambazo zinaweza kukusaidia kuzuia UTI, nazo ni hizi:
- Maji Ni Rafiki Mzuri Kwako: Kunywa maji mengi na kutumia vinywaji ambayo huondoa sumu. Maji hufafifisha mkojo na kuufanya kuwa na tindikali kidogo na kuwa na rangi nyeupe kama maji. Kwa njia hii, mtu hatapata maumivu ya tumbo au muwasho wakati wa kukojoa.
- Fanya Usafi: Epuka kutumia vyumba vya mabafu ya pamoja kwani maambukizi huenea mara kwa mara katika huduma za kawaida. Unapaswa kujitawaza kutoka mbele kwenda nyuma ili kuzuia bakteria wanaokuwa maeneo ya njia ya haja kubwa wasiingie kuingia kwenye uke au njia ya mkojo.
- Kukojoa Mara Kwa Mara: Usibane mkojo. Tumia bafu kila unapohisi kwenda kukojoa. Hii sio tu itatoa sumu, bali pia itaondoa uzito wa kibofu cha mkojo na kukupa utulivu kutokana na maumivu ya tumbo.
- Nguo Ya Ndani Nzuri: Usivae chupi zinazobana kwani bakteria hukaa katika mazingira yenye unyevunyevu na joto. Badilisha nguo zako za ndani mara kwa mara na udumishe usafi wako.
- Epuka kutumia sabuni zenye marashi makali, cream, dawa za kuoshea ukeni, au kupulizia poda. usafi wa kike na poda
Je, Suluhisho Lake Ni Nini?
James Herbal Clinic tunazo dawa nzuri zenye uwezo
mkubwa wa kuondoa kabisa maambukizi ya UTI, nazo ni PERFECT POWDER, FRESH HERB
na CARD HERB
Ndugu rafiki makala yetu naomba iishie hapa, nikaribishe kipindi cha maswali na maoni yako. Pia unaweza kutuma namba yako ya WhatsAp tuweze kukuunganisha na darasa letu la mafunzo ya afya.
Je, Unahitaji Huduma? Basi wasiliana nasi kwa namba hizi: 0768 559 670/0712 181 620,
Arusha-Mbauda,
Karibu sana!
Comments
Post a Comment