Fahamu Dalili 7 Za Kushuka Kwa Viwango Vya Homoni Ya Testosterone Kwa Mwanaume.

Kushuka kwa homoni ya Testosterone ni hali ambapo korodani hushindwa kutoa au kuzarisha homoni ya kutosha. Korodani ni viungo vya uzazi  katika mfumo wa uzazi kwa mwanaume.

Testosterone ni homoni ya uzazi ya mwanaume na ina idadi ya majukumu muhimu ikiwa ni pamoja na ukuzaji wa sifa za pili za jinsia na kudumisha utendaji kazi wa tezi dume na viasili vya shahawa au mbegu za mwanaume.

Kwa kawaida viwango vya homoni ya Testosterone huanza kushuka kwa wanaume takribani walio na umri wa miaka 30-40. Zipo sababu nyingine zinazopelekea viwango vya homoni ya testosterone kushuka chini, ambayo hata hivyo vinaweza kusababisha kuonekana kwa dalili.

Je, Nini Husababisha Kushuka Kwa Viwango Vya Homoni Ya Testosterone Kwa Wanaume?

Upungua huanza kwa kiwango cha asilimia 1% kwa mwaka, na hii haiwezekani kusababisha matatizo yoyote. Hata hivyo, kuna sababu nyingine zinazopelekea kushuka kwa homoni ya testosterone, ambayo inaweza kusababisha dalili. Hizi zinaweza kuainishwa kama mapungufu ya awali ya homoni ya testosterone na mapungufu ya pili pia.

Upungufu Wa Awali Wa Homoni Ya Testosterone

Aina hii ya kushuka kwa viwango vya homoni ya testosterone husababishwa na korodani kushindwa kutengeneza homoni ya testosterone ya kutosha. Hali hii inaweza kutokana na:

  • Kuumia kwa korodani
  • Kufanyiwa upasuaji kwa korodani
  • Korodani kuwa ndogo
  • Ugonjwa wa kurithi unaosababisha kunyonya madini ya chuma mengi, nk

Upungufu Wa Pili Wa Homoni Ya Testosterone

Kwa aina hii ya kushuka kwa homoni ya testosterone korodani huwa ni za kawaida lakini hazina uwezo wa kuzarisha  homoni ya testosterone ya kutosha kwa sababu ya tatizo na sehemu nyingine za mwili, kwa mfano, tezi ya pituitari au hypothalamus. Hizi zinaweza kuwa na uwezo mdogo kutokana na:

  • matatizo ya tezi ya pituitary
  • ukimwi
  • baadhi ya matibabu ya homoni, nk

Kama Mwanaume, Je Unawezaje Kufahamu Kama Una Kiwango Cha Chini Cha Homoni Ya Testosterone?

Njia pekee ya kujua kwa uhakika kama una viwango vya chini vya homoni ya testosterone ni kupima viwango vyako kwa kipimo cha damu. Unaweza kufanya kipimo cha damu mwenyewe nyumbani, au unafika kituo cha afya mahali popote unapokuwa.

Je, Dalili Za Kiwango Cha Chini Cha Homoni Ya Testosterone Kinakuwaje

Kiwango cha chini cha homoni ya mara nyingi huwa hakisababishi dalili za kimwili. Hata hivyo, kuna kiwango cha dalili zinazohusiana na viwango vya chini vya homoni testosterone, navyo ni pamoja na:

  • kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa
  • kupungua kwa nguvu za kiume
  • nywele kunyonyoka
  •  misuli ya mwili kuwa laini
  • kuhisi uchovu
  • kuwa na mwili mnene/mwembamba
  • msongo wa mawazo

Dalili hizi zinaweza kuwa ni matokeo ya magonjwa mengine pia, kwa hivyo ikiwa unakumbana na yoyote kati ya yaliyo hapo juu na una wasiwasi, unapaswa kufika hospitalini ili kupata uchunguzi zaidi ili ujue vyanzo vyake.

Je, Kushuka Kwa Viwango Vya Homoni Ya Testosterone Kunatibikaje?

James Herbal Clinic tunatibu ugonjwa au tatizo hili kwa kutumia dawa za asili pamoja na tiba lishe zenye kiwango kikubwa cha virutubishi.

Makala yetu inaishia hapa, naomba nikaribishe kipindi cha maswali na maoni yako. Pia unawa kutuma namba yako ya WhatsAp ili tuweze kukuunganisha kwenye darasa letu la masomo ya afya.

Je, Unahitaji huduma? Basi, wasiliana nasi kwa namba hizi: 0768 559 670/0712 181 626,

Arusha-Mbauda,

Karibu sana!

 

Comments

Popular posts from this blog

Aina 9 Ya Vyakula Unavyopaswa Kuviepuka Unapokuwa Na Tatizo La Figo

Fahamu Mambo Yanayosababisha Uke Kulegea

Mambo 6 Yanayopelekea Mwanamke Kuhisi Maumivu Makali Anaposhiriki Tendo La Ndoa