Fahamu Faida Za Unga Lishe Bora Wa NUTRI-REDEEMER
NUTRI-REDEEMER ni unga bora wa pekee uliotengenezwa kutokana na mchanganyiko wa vyakula vya nafaka, mbegumbegu na mbogamboga zenye virutubisho vingi vizuri tena vyenye afya bora mno. Moja ya mchanganyiko wa nafaka hizo ni ngano.
Unga huu
unatumiwa kwa ajili ya uji kwa mtu mzima na watoto pia na una faida nyingi sana
kama hizi zifuatazo:
- kudhibiti uzito wa mwili,
- kuboresha mfumo wa homoni kwa mwanamke na mwanaume,
- kuboresha mbegu za mwanaume,
- kuondoa matatizo ya macho,
- kuzuia magonjwa ya moyo,
- kisukari na saratani,
- kuboresha ubongo,
- ngozi, na mifupa,
- kuboresha uyeyushaji wa mafuta mwilini mwako,
- kuzuia mawe kwenye figo,
- kuzuia saratani ya matiti,
- kurekebisha mfumo wa uzazi wa mwanaume na wa mwanamke, nk.
Unga huu pia
huzuia mwili usipatwe na magonjwa ya saratani ya utumbo, hutuliza dalili za
kukoma kwa hedhi na kuzuia mashambulio ya moyo. Kwa kutumia unga huu kama lishe
mara kwa mara, basi unaweza kupata virutubisho vyote vilivyomo na kuzuia
kutokea kwa magonjwa mbalimbali.
Je, Ngano Ni
Nini?
Ngano ni nafaka ya kawaida kabisa na
inapatikana karibia katika kila mahali. Utaipata kwenye mkate, keki, mandazi,
chapati japokuwa wengi hutumia unga wa ngano iliyokobolewa ambayo haina faida
hata kidogo.
Nafaka ya ngano ya asili yenye afya
hutegemea zaidi aina ya nafaka inayotumika kama chakula chenye afya kwa
mwanadamu. Kwa mfano ngano ambayo haijakobolewa inachukuliwa kuwa mojawapo ya
aina bora zaidi ya ngano, hivyo basi, ngano inapokobolewa na kuondolewa tabaka
la juu, afya yake huondolewa kabisa. Tabaka hili huwa lina virutubisho vingi
mbalimbali kama vile Vitamini B3, B2, B1, folic acid, shaba(copper), chokaa(calcium),
zink, nyuzinyuzi(fiber), Pamoja na chuma(iron), na unapovikosa hivi kwenye mlo
wako unaweza kuwa na matatizo baadaye.
Ngano ina virutubishi vingi sana ambavyo
vinafaa kwa afya ya mwili wako. Hivyo basi, NUTRI-REDEEMER ina Vitamini E, B,
madini ya chuma, shaba, chokaa, iodide, magnesium, zink, potassium, manganese,
Sulphur, silicon, chlorine, ndio maana ni msingi mzuri wa lishe yoyote
unapoitumia.
Thamani Ya Virutubisho Vya Ngano Kwenye Unga
Wa NUTRI-REDEEMER
James Herbal Clinic tumekuandalia unga huu kama
chakula lakini pia ni dawa tena ni chakula chenye vurutubisho vingi vya kutosha
kwa ajili ya afya ya mwili wako. Ninavyoelezea hapo chini ni faida ya afya bora
ya mwili wako kutoka na NUTRI REDEEMER.
1. Kudhiti
Uzito Wa Mwili
Ingawa ngano inafahamika kwa kudhitibi uzito
wa mwili, kwahiyo NUTRI-REDEEMER ina nguvu sana kwa wanawake na wanaume.
Unapoitumia kama chakula tena ni dawa, inasaidia sana kupunguza uzito wa mwili
hasa unene au kitambi.
2. Huboresha Kazi Ya Uyeyushaji Mafuta
Mwilini
Wakati kazi ya uyeyushaji mafuta mwilini
inaposhindwa kufanyika, inaweza kupelekea kuwapo kwa mvurugiko wa mafuta.
Baadhi ya mvurugiko huo ni mlundikano wa mafuta na hivyo kusababisha kitambi,
shinikizo la juu la damu, nk. Hali hii inaweza kumfanya mgonjwa kuwa katika
hatari ya magonjwa ya moyo.
Hii ndio maana James Herbal Clinic
tunakushauri ubadiri mitindo ya ulaji wako, huku ukitumia NUTRI-REDEEMER kama
chakula n ani dawa. Kwahiyo huboresha mmeng’enyo wa chakula wote, ambao
hupelekea uunguzaji wa mafuta kuwa mzuri, na hivyo kuzuia matatizo haya
yasiibuke katika sehemu ya mwanzo.
3. Huboresha Mbegu Za Mwanaume
Mbegu nyepesi za mwanaume inamaanisha kwamba
manii unayoitoa wakati unapofika kileleni huwa ina mbegu chache mno kuliko
kawaida. Kiwango chako cha mbegu huonekana kidogo kuliko kawaida ikiwa kama una
mbegu milioni 15 kwa milimita za shahawa.
Hivyo, NUTRI-REDEEMER husaidia kabisa
kuboresha mbegu za mwanaume kuwa nzito tena nyingi endapo kama utaitumia kama
chakula na dawa.
4. Huzuia Kisukari Aina Ya Pili
Pale ugonjwa wa kisukari aina ya pili
unapokuwa ugonjwa sugu, na unaweza kuwa hatari kabisa kama haudhibitiwi vizuri,
pia ni ugonjwa ambao unaweza kubadirishwa ikiwa kama mgonjwa atajari mlo wake.
Moja ya virutubishi vinavyopatikana kwa wingi katika NUTRI-REDEEMER ni
magnesium.
Madini haya ni kipengele cha ushirikiano
Zaidi ya vimeng’enya 300 ambavyo huathiri moja kwa moja jinsi mwili unavyotumia
insulin na kutengeneza sukari. Hivyo, ukitumia NUTRI-REDEEMER kwa utaratibu
unaotakiwa itakusaidia kudhibitisukari kwenye damu yako. Kwa kubadirisha tu
vyakula vya wanga ukaachana navyo kabisa, ukatumia unga huu bora wa lishe,
mgonjwa wa kisukari unaweza kudhibiti viwango vya sukari kwa urahisi mno.
5.Huzuia Saratani Ya Matiti
NUTRI-REDEEMER inazuia saratani kwa wanawake,
ambayo humaanisha kwamba huyeyusha na kuondoa madhara ya saratani na kuzuia
aina mbalimbalia za saratani. Wakati viwango vya homoni ya estrogen
vinapoongezeka na kujaa, ndipo husababisha saratani kwenye matiti. Wakati mbegu
za nafaka zinapoongezeka na kuchochea viwango vya homoni ya estrogen kiasi
kwamba hudhibitiwa muda wote, ndipo huzia saratani ya matiti.
Lishe hii hasa inafaa kwa wanawake walio
katika kipindi kabla ya kuanza kukoma hedhi, ambao kwa kawaida wapo katika
hatari ya kupatwa na saratani ya matiti. Zaidi ya hapo, ngano iliyo kwenye
NUTRI-REDEEMER pia ina kundi la molekuli. Kwahiyo kundi la molekuli huchukua
vipokezi vya homoni vinavyokuwa mwilini, ambavyo pia husaidia kuhifadhi
mzunguko mkubwa wa viwango vya estrogen unaoangaliwa, ambao pia husaidia kuzia
saratani ya matiti.
6. Huondoa Tatizo La Kukosa Choo
Kama nilivyoeleza hapo awali, NUTRI-REDEEMER
ina wingi wa nyuzinyuzi au fiber na husaidia choo kuwa laini. Hii humaanisha
kwamba mwili huhitaji uzarishaji wa asidi kidogo ya nyongo ili kuyeyusha
chakula tumboni na kukifanya kuwa laini. Matokeo yake ni kwamba, kinyesi au
choo unachotoa kinakuwa nil aini. Hali hii inaweza kuzuia saratani ya utumbo
mpana isiweze kutokea na kuufanya utumbo mwembamba kuwa wenye afya hasa kwa
wanawake.
7. Hutuliza Dalili Kabla Ya Hedhi Kukoma
Unapotumia mlo wenye wingi wa nafaka asili
inafaa mno kwa wanawake waliofikia ukomo wa hedhi kadiri wanapoelekea kuwa
katika ahatari ya magonjwa mbalimbali. NUTRI-REDEEMER itakusaidia sana
unapokuwa na tatizo la shinikizo la juu la damu, ugonjwa wa moyo, na mwili kuwa
na mafuta mengi ambayo husababisha mishipa ya damu kuwa na mafuta na kuwa
migumu. Kwahiyo itakusaidia mno kuepukana na magonjwa ya kiharusi au shambulio
la moyo.
8. Huzuia Shambulio La Moyo
Zaidi ya mara nyingi, madaktari hupendelea
kuwashauri wagonjwa wa shambulio la moyo kutumia tiba za asili ili waweze
kupona ugonjwa huo. Hii ni kwasabbau tiba hizi za asili hufanya kazi haraka
kuponya magonjwa haya. Japokuwa haijulikani kwanini dawa za asili hufanya kazi
vizuri kuliko madawa ya vidonge, ndio maana madaktari huhimiza matibabu ya
vyakula na dawa za asili.
Vyakula vya nafaka kama vile ngano iliyopo
kwenye NUTRI-REDEEMER na mchanganyiko wa vyakula vingine vyenye
nyuzinyuzi(fiber), husaidia sana kupunguza kiwango cha shinikizo la juu la
damu(high blood pressure) kwa mgonjwa, na hivyo kupunguza hatari ya kupatwa na
shambulio la moyo. Kusema kweli, tiba za asili kama lishe huambatana na
mapendekezo yote ya mazoezi yanayotakiwa ili kuondoa tatizo la moyo.
Nashukuru sana mpendwa msomaji wa Makala hii kuhusu faida za NUTRI-REDEEMER, ni chakula bora kwa afya yako pia ni dawa kwa magonjwa makubwa mwilini mwako.
Sasa unaweza kuagiza na itakufikia mahali popote mikoani.
Je, Unahitaji Huduma? Basi tupigie
0768 559 670 au 0712181626,
Arusha-Mbauda,
Karibuni sana.!
.
Comments
Post a Comment