Fahamu Sababu Zinazopelekea Wanawake Wengi Kushindwa Kupata Mimba
Hali ya ugumba inatafsiriwa kama vile mwanamke kutokushika ujauzito angalau mara moja kwa mwaka japokuwa anafanya tendo la ndoa kila mara lakini bila mafanikio. NUKUU: Visababishi vya ugumba wa mwanamke vinaweza kuwa vigumu sana kuvipima na kuvitambua. Zipo tiba nyingi sana ambazo zinategemeana na chanzo cha ugumba. Wanandoa wengi wenye matatizo ya ugumba wanaweza wakafanikiwa kupata ujauzito hata bila kutumia tiba. Je, Dalili Zake Zinakuwaje? Dalili kuu za tatizo la ugumba kwa mwanamke ni kutokuwa na uwezo wa kupata ujauzito. Mzunguko wa hedhi ambao huwa mrefu(yaani siku 35 na zaidi), au mfupi(yaani chini ya siku 21), au mzunguko wa kubadirika badirika au kutokuona hedhi kabisa inaweza kumaanisha kwamba huna uwezo wa kupevusha mayai. Kunaweza kusiwepo na dalili zozote za nje. Je, Nini Husababisha Hali Ya Ugumba Kwa Mwanamke? Kwanza kabisa ni urutubishaji na upandikizaji wa yai kwenye ukuta wa mfuko wa uzazi. Mambo hayo ni ya muhimu sana ili kumfanya mwanamke kuwa mjam...