Posts

Showing posts from October, 2024

Haya Ndio Mambo 6 Yanayofanya Mirija Ya Uzazi Kuziba

Image
Hali ya kujaa maji kwa mirija ya uzazi ya wanawake huitwa kitaalamu, “hydrosalpinx”. Ni tatizo ambalo hujitokeza kwa wanawake kutokana na maambukizi ya magonjwa ya zinaa ambayo yamekaa muda mrefu bila kutibiwa, kama vile kisonono, pangusa, malengelenge, nk, ambayo kwa ujumla tunaweza kuita maambukizi katika via vya uzazi yaani PID (pelvic inflammatory disease),  bila shaka tutayazungumzia baadaye katika makala zinazofuata kwa kuchanganua ugonjwa mmoja baada ya mwingine na tutaona madhara yake na dalili zake pia. Mara nyingi matatizo haya husababisha tatizo la ugumba na maumivu ya kiuno. NUKUU: Mirija ya uzazi hujishikiza upande wa kulia na kushoto mwa tumbo la uzazi, nayo hupitisha mayai kila mwezi kutoka kwenye ovari ama kifuko cha yai, kwenda kwenye mji wa uzazi. Urutubishaji wa yai la uzazi hutokea katika mirija hii. Je, Nini Chanzo Cha Mirija Ya Mayai Kuziba? Mara nyingi mirija ya uzazi kuziba hutokana na magonjwa mengi nayo huwa kama ifuatayo ; Maambukizi katika via vya uzazi ...

Mambo 6 Yanayomfanya Mwanamke Kuhisi Maumivu Ya Tumbo Wakati Wa Hedhi Au Baada Ya Kutoka Hedhini

Image
Wanawake wengi huhisi maumivu ya tumbo kabla au wanapokuwa hedhini. Lakini inaweza pia mwanamke akahisi maumivu ya tumbo anapokuwa hedhini. Maumivu haya mara nyingi huwa sio makali sana. Hata hivyo, ni muhimu kwamba unayafuatilia, hasa ikiwa kama yanakaa kwa muda mrefu. Maumivu ya tumbo wakati wa hedhi inaweza kuwa ni dalili ya magonjwa mbalimbali. Endelea kusoma Makala hii ujifunze dalili, visababishi, Pamoja na matibabu ya kukosa hedhi au kutokwa na damu ya hedhi nyingi kwa muda mrefu. Je, Nini Visababishi Vyake? Wakati mwingine maumivu ya tumbo baada ya hedhi huwa sio makali mno. Lakini kama una maumivu makali endelevu yanayodumu muda mrefu kuliko mzunguko wako wa hedhi, inaweza kuwa ishara kwamba una magonjwa kwenye tumbo lako la uzazi(uterus). Hapa nitakuelekeza visababishi vya maumivu ya tumbo unapotoka hedhini: 1.  Endometriosis Endometriosis ni ugonjwa ambao hutokea pale seli zinazofanana na ukuta laini wa mji wa mimba ( uterus) zinapoota nje ya mji wa mimba. Ugonjwa huu u...

Jinsi Ya Kuandaa Chapati Ya Brown Ya Kusukuma.

Image
Chapati ya brown ni chapati inayoandaliwa kwa kutumia unga wa ngano ambayo haijakoborewa kama unavyoona kwenye picha hapo chini. Je, Unaandaaje Chapati Hii?   MAHITAJI Unga wa ngano kilo 1 Mafuta ya kupikia au siagi vijiko vya chakula (tablespoon) 10 Sukari au asali kijiko 1 cha chakula Chumvi kijiko cha chai 1 Tui la nazi vikombe 3 na nusu Mafuta ya kukaangia nusu lita F aNUKUU: Ili kuifanya chapati iwe laini, chukua unga wa ngano ambayo haijakobolewa nusu kilo na unga wa ngano mweupe nusu kilo ili upate kilo 1.  HATUA ZA KUFUATA  Pima unga wa ngano na uchekeche vizuri Weka chumvi, sukari au asali, tui la nazi na mafuta uchanganye vizuri, Kanda unga kwa tui la nazi kwa dakika 8-10 au mpaka ulainike kabisa. Kata madonge ya duara kwa kukadiria au pima gramu 120 kwa kila chapati. Sukuma umbo duara kwa donge, paka mafuta kijiko kimoja cha chakula, kunja. Fanya hivyo kwa madonge yote. Funika ziache kwa dakika 7 Weka kikaangomotoni na sukuma chapati duara la saizi ya kati. We...

Zijue Sababu Zinazofanya Uke Kutoa Sauti Wakati Unaposhiriki Tendo La Ndoa

Image
Uke kutoa sauti ni pale hewa inapopita na kuingia ndani ya uke. Hewa inapopita, baadaye hutoka ukeni na inaweza kusababisha sauti sawa na kujaa gesi tumboni na kutoka kwenye njia ya haja kubwa(kujamba). Kwa kawaida ni tukio la kawaida, na huwa ni hali inayojitokeza kwa nadra sana.  NUKUU: Hata hivyo inaweza kuwa ni dalili ya ugonjwa ambao utahitaji kutibiwa.  Ngoja tuangalie vyanzo vyake na ni wakati gani unapaswa kufika hospitali kuweza kupata matibabu. Je, Visababishi Vyake Ni Nini? Kuna mambo mengi mbalimbali yanayoweza kusababisha uke kutoa sauti. Ni vyema kufahamu vyanzo mbalimbali, kwani mengine yanahitaji kushughulikiwa na mtaalamu wa matibabu. Baadhi ya vyanzo hivi ni kama hivi vifuatavyo; 1.  Kushiriki Tendo La Ndoa Tendo la ndoa ni chanzo cha uke kutoa sauti. Mwendo wa uume unapoingia ndani na kutoka nje wakati mwingine unaweza kusababisha hewa kuingia na kisha kuzuiwa. Wakati misuli ya uume inapotuna kutokana na kumwaga shahawa au pale uume unapotolewa nje, bas...

Haya Ndio Mambo Yanayomfanya Mwanaume Au Mwanamke Kushindwa Kupata Mtoto

Image
Katika suala zima la ugumba kwa mwanaume na mwanamke lazima kuwepo na vigezo vya uchunguzi. Kwa mwanamke mambo ya kuangalia ni historia yake katika matumizi ya madawa ya tiba alipokuwa mdogo au hata kama mama yake aliwahi kutumia aina fulani za madawa wakati wa ujauzito. Wataangalia kama ulivunja ungo kwa wakati muafaka, mfano uliwahi sana au ulichelewa sana. Muda muafaka ni kati ya miaka 12 hadi 16. Kufahamu mzunguko wako wa hedhi unavyoenda na kiwango cha damu unachopata, kama ulishawahi kutumia njia za kisasa za uzazi wa mpango. Je, ulishawahi kupata mimba? Na ulizaa au iliharibika? Je, uliwahi kutoa mimba? NUKUU: Vile vile inahitajika kujua kama ulishawahi kufanyiwa upasuaji wowote chini ya tumbo mfano kutoa uvimbe, mimba nje ya kizazi, kuzaa mtoto kwa upasuaji. Ni muhimu pia daktari akafahamu endapo ulishawahi kupata maambukizi yoyote katika viungo vya uzazi(PID), madawa uliyokwishawahi kutumia kwa muda mrefu, ulaji wako wa vyakula, kama unakunywa pombe au unavuta sigara. Je, Kwa...

Kuondoa Sumu Mwilini: Kwanini Ni Jambo La Muhimu Sana?

Image
Ulimwengu wa siku hizi, sumu imekuwa jambo la kutia wasiwasi sana  kutokana na ukweli kwamba mtindo wa maisha wa leo  unasababisha sumu  kujilimbikiza   katika  miili yetu.  Sababu kuu zinazosababisha mkusanyiko huu wa sumu ni mchafuko wa hewa na maji, kemikali kali zaidi, mionzi na nguvu za nyuklia.  Vilivyoongezwa tena katika jambo hili ni kemikali mpya, madawa,  amba y o watu wanameza , matumizi ya sukari, vyakula vilivyo kobolewa au kusindikwa , nyama na samaki na vichocheo vya madawa wanayotumia wanyama. :Sumu ni tatizo kubwa sana leo na inaweza kusababisha magonjwa.   Kansa , magonjwa mengine ya moyo na mishipa yamekuwa yakisababishwa na mkusanyiko wa sumu mwilini. Magonjwa mengine, mizio, unene au kitambi , matatizo ya ngozi, baridi yabisi au gauti ( arthritis )  na mengine   yanayohusiana na afya.Pia mrundikano wa sumu hupelekea mara kwa mara   maumivu ya kichwa, uchovu  wa mwili , matatizo ya tumbo, maumivu ya mwi...

Fahamu Mambo 9 Yanayosababisha Tumbo Kutokusaga Chakula.

Image
  Rafiki , na ieleweke kuwa hali ya chakula kutokumeng’enywa tumboni mwako sio ugonjwa, bali ni baadhi ya dalili zinazokupata, kwa mfano;  tumbo kuuma na kujaa gesi mara baada tu unapoanza kula chakula. Ingawa tatizo hili linaonekana kuwa la kawaida sana, lakini tatizo hili linaweza kutokana na vyanzo mbalimbali. Dalili za chakula kutokumeng’enywa unaweza kuzihisi mara kwa mara kila siku. NUKUU: Hali ya kutokumeng’enywa kwa chakula tumboni inaweza kuwa dalili ya ugonjwa mwingine wa usagaji chakula tumboni mwako. Je, Nini Dalili Za Tatizo Hili? Watu wengi wenye tatizo hili wanaweza kuwa na dalili moja au zaidi, nazo huwa kama ifuatavyo: Tumbo kujaa gesi wakati anapokula chakula Tumbo kujaa gesi muda mrefu Kuhisi maumivu ya tumbo la juu Kuhisi kiungulia juu ya tumbo Tumbo kuunguruma sana mara kwa mara na kuhisi maumivu chini ya kitovu Kuhisi kichefuchefu na kutaka kutapika Wakati mwingine watu wanaosumbuliwa na tatizo hili pia hupatwa na kiungulia, lakini kumbuka kuwa kiungulia ...

Haya Ndio Baadhi Ya Aina Ya Magonjwa Ya Kibofu Cha Nyongo

Image
  Je, Unazifahamu Kazi Za Kibofu Cha Nyongo? Kibofu cha nyongo kina urefu wa inchi 4, na ni kiungo chenye umbo la peasi. Kiungo hiki kiko chini ya ini sehemu ya juu ya tumbo lako. Kibofu hiki huhifadhi nyongo, mchanganyiko wa majimaji, mafuta, pamoja na lehemu (cholesterol). Nyongo husaidia kuyeyusha mafuta yanayokuwa kwenye chakula chenye mafuta pale kinapoingia tumboni mwako. NUKUU: Kibofu cha nyongo hutoa nyongo na kuiingiza kwenye utumbo mwembamba. Hali huruhusu vitamini za  mafuta mumunyifu (fat-soluble vitamins) pamoja na virutubishi kuweza kunyonywa kwa urahisi  na kuingizwa kwenye mkondo wa damu. Je, Dalili Za Matatizo Ya Kibofu Cha Nyongo Zinakuwaje? Matatizo ya kibofu cha nyongo huwa yanakuwa na dalili zenye kufanana. Dalili hizi huwa  kama ifuatavyo; 1. Maumivu Dalili ya kwanza kabisa ya kibofu cha nyongo huwa ni maumivu. Maumivu haya kwa kawaida hujitokeza katikati pembeni mwa tumbo lako kuelekea juu. Yanaweza kuwa maumivu ya kawaida au ya kwend...

Fahamu Vyanzo 7 Vya Ugonjwa Wa Fangasi Sehemu Za Siri Kwa Wanawake

Image
  Je, Maambukizi Ya Fangasi Ni nini?   Candida albacans ni vimelea wa fangasi ambao hukua kama fangasi ama seli zenye kusababisha kuwepo kwa maambukizi ya fangasi kwa mwanadamu. Fangasi ya asili ijulikanayo kama Candida albicans, mara nyingi husababisha aina hii ya kuvimba kwa uke(Vaginitis). Kama inavyokadiriwa kuwa katika wanawake wanne, basi watatu wanaweza kuwa na maambukizi ya fangasi katika maisha yao,  haijalishi una umri gani. Hapo awali ilionekana kuwa jambo la kawaida sana mwanamke kuwa na maambuki ya fangasi sehemu za siri, lakini leo inaonekana kuwa tatizo la kutisha kwani linaweza kuzarisha madhara mengine makubwa ambayo muhusika hakutarajia kama vile kuvimba ukeni, muwasho na masumbufu mbalimbali. NUKUU: Magonjwa ya maambukizi yamekuwa yakienea kwa njia mbalimbali hasa kwa njia ya kujamiiana. Kwa upande mwingine maambukizi haya sio kwamba ni magonjwa ya zinaa tu. Wagonjwa wamekuwa wakipatwa na masumbufu mengi katika kutibu maambukizi katika via vya uzazi h...

Angalia, Mwezi Mmoja Kabla Ya Kiharusi, Mwili Wako Utakutumia Ishara Hizi za Tahadhari!

Image
Katika nafasi ya kwanza unaweza kutaka kujua kiharusi kinatokana na nini. Ni " shambulio la ubongo" ambalo hutokea wakati mtiririko wa damu kwenye sehemu ya ubongo inpoingiliwa. Katika makala hii tutazungumzia kuhusu viharusi, ishara za kawaida za tahadhari na jinsi ya kujikinga. Kwanza, unapaswa kujua kwamba kuna aina 2 kuu za viharusi: ischemic na hemorrhagic . Viharusi vya Ischemic ni kawaida zaidi na husababishwa na kupungua au kuziba kwa mishipa kwenye ubongo, na kusababisha kupungua kwa mtiririko wa damu. Viharusi vya hemorrhagic sio vya kawaida sana na husababishwa na damu kuvujia kwenye ubongo. Kumbuka: unapaswa kujua kwamba ni muhimu sana kutambua ishara za za ugonjwa wa kiharusi na kupata msaada wa matibabu haraka iwezekanavyo ili kupunguza hatari ya uharibifu mkubwa kwenye ubongo. Hii inaweza kusaidia kupunguza hatari ya kifo au ulemavu na kuboresha uponyaji wako. Wataalamu hao wa matibabu wanasema dalili na ishara  zinaweza kutofautiana kutoka kwa mtu mmoja hadi ...

Haya Ndio Mambo 8 Yanayopelekea Mzunguko Wako Wa Hedhi Kubadirikabadirika!

Image
Ieleweke hivi, ingawa mzunguko wa hedhi wa wastani huwa siku 28, lakini unaweza kuonekana pia siku 24 au kila baada ya siku 34. Baada ya kubalehe, wanawake wengi huwa na mzunguko wa hedhi usiobadirika hata kidogo; lakini baadhi yao hubaki katika mzunguko wenye tabia ya kubadirika badirika. NUKUU: Kutokwa damu ya hedhi kwa kawaida huwa ni siku 3-4, na wastani wa siku 5 ambao kitaalam ndio huonekana kuwa mwanamke anachukuwa muda mrefu akitokwa damu ya hedhi.   Je, Nini Visababishi Vyake? Mzunguko wa hedhi kubadirika badirika mara nyingi husababishwa na mambo yafuatayo: Vichocheo kutokuwa na uwiano sawa (hormone imbalance) Msongo wa mawazo Wasiwasi Mazoezi mazito Kuporomoka kwa mimba. Matumizi ya madawa hasa madawa ya uzazi wa mpango, nk. Magonjwa sugu kama vile ya zinaa, kisukari au magonjwa ya moyo, nk Magonjwa katika mfumo wa uzazi hasa vivimbe kwenye vifuko vya mayai, mji wa mimba(Uterus), mirija ya mayai, kuharibika kwa ukuta wa kifuko cha uzazi, nk Je, Dalili Zake Zinakuwaje? ...