Posts

Showing posts from November, 2024

Unaweza Kuyashinda Magonjwa Na Dhambi Kupitia Nguvu Za Mungu

Image
Amini Sana Nguvu Za Mungu Hebu tufungue kitabu cha Yoshua, sura ya 11. Miaka iliyopita, mara nyingi nimekuwa nikijifunza  kuhusu watu wa Israeli na jinsi gani walivyoingia katika nchi ya Kanaani. Niliona usambamba wa watu wa Mungu katika siku hizi za mwisho na kuingia kwao katika Kanaani ya Mbinguni. Nilijifunza kuachiliwa kwao kutoka utumwani Misri na kuchelewa nyikani. Niliona ulinganifu wa kutolewa kwa Watu wa Mungu kutoka Babeli na kuchelewa kwao nyikani. Niliona uzoefu wa Waisraeli wa kupanda na kushuka  na wangapi kati yao waliokufa nyikani. Kisha nimejifunza jinsi walivyopita katika mto Yordani na pia njia yao karibu na Edomu, ambayo tena ilikuwa hadithi ya kuvutia.   Ningependa kuendeleza hadithi ambayo kwa sehemu fulani hatujazingatia sana, lakini ambayo inatuhusu sisi leo, na hiyo ndiyo sehemu inayopatikana katika kitabu cha Yoshua. Sura chache za kwanza zinahusu zaidi ushindi wa mji mkuu ambao ulikuwa Yeriko. Kisha hadithi inakwenda kwenye ushindi wa Ai, kipind...

Fahamu Vyanzo Na Dalili Za Uric Acid

Image
Je, Nini Maana Ya Uric Acid? Uric acid ni uchafu au  taka iliyobaki kutokana na michakato ya kawaida ya kemikali katika mwili, nayo hupatikana kwenye mkojo na damu. Mkusanyiko usio wa kawaida wa uric acid mwilini unaweza kusababisha ugonjwa unaoitwa gout. Kuongezeka kwa viwango vya uric acid kwenye damu na mkojo inaweza kuwa athari.   Kiwango cha juu cha uric acid kwenye  mkojo huwa ni uric acid nyingi k wenye damu. Uric acid hutengenezwa wakati  wa ku meng’enywa  kwa chembechembe ngumu . Chembechembe ngumu  hupatikana katika vyakula fulani na huundwa na mwili. Damu hupeleka uric acid  kwenye figo. Figo hupitisha  uric acid nyingi kwenye mkojo, ambayo baadaye hutoka mwilini . Kiwango cha juu cha uric acid  kinaweza ku sababishwa na gout au mawe kwenye figo. Lakini watu wengi walio na viwango vya juu vya uric acid  hawana dalili za mojawapo ya hali hizi au matatizo yanayohusiana  tatizo hili . Je, Nini Chanzo Chake? Kiwango cha juu c...

Je, Inafaa Mwanamke Kuwa Na Tumbo Kubwa?

Image
Wanawake wengi miaka ya karibuni wanakabiliwa na tatizo linalofanana na kitambi kwa upande wa wanaume. Hivyo ingekuwa ni wanaume tungesema ni kitambi ambalo nalo ni tatizo kubwa miongoni mwa wanaume wengi nyakati za sasa. Kinachowasumbuwa wanawake siyo kitambi tunasema ni mlundikano wa mafuta sehemu ya chini ya tumbo na tumbo kwa ujumla kufikia hali kuonekana kama ana tumbo kubwa au kuhisi labda ni ujauzito kumbe ni mafuta tu mengi. Kwa ujumla ni vigumu sana kupunguza tumbo la namna hii, hivyo kwenye post hii pamoja na mengine tutaona pia visababishi vya tatizo lenyewe, dawa za asili zinazoweza kuondoa tatizo hilo na aina ya maisha unayotakiwa kuishi ili ufanikiwe kirahisi zaidi bila kukuachia madhara mengine yoyote. Nini kinasababisha tumbo kwa kina mama: Vyakula feki (Junk food) Kutumia vyakula vya wanga kupita kiasi Kutokunywa maji ya kutosha kila siku Kula chakula kizito muda mchache kabla ya kwenda kulala Kukaa masaa mengi kwenye kiti Kutokujishughulisha na mazoezi Mfadhaiko (stre...

Haya Ndio Makundi Ya Vyakula Vilivyokaangwa Vinavyosababisha Wanaume Wengi Kupungukiwa Nguvu Za Kiume.

Image
Moja ya njia sahihi za asili katika kutatua tatizo la kupungukiwa nguvu za kiume ni kuanza kurekebisha mtindo wa ulaji na unywaji hata kama unatumia tiba au bidhaa kutoka James Herbal Clinic. Kufanya hivi ni kujiepusha na milo inayosababisha kupungukiwa nguvu za kiume ikiwa pamoja na uchafu wa mazingira, kemikali ambazo zinaonekana kudhoofisha mfumo wa uzazi wa mwanaume.  NUKUU: Kwa nyongeza, unaweza ukaanza kujifunza ili kuona mambo mengine ya kimitindo yanayoweza kusababisha kupungukiwa nguvu za kiume ikiwa pamoja na vyakula au milo inayoweza kujenga afya yako katika kurejesha nguvu za kiume na kukufanya kuwa mwenye hisia katika tendo la ndoa. 1.  Epuka Vyakula Vya Nyama Mafuta ya wanyama pamoja na kolestero kwakweli yanaonekana kuwa mabaya kwa afya ya mfumo wa moyo wako. Hata hivyo unatakiwa ujenge afya yako iwe bora zaidi ikiwa kama unahitaji kufurahia kitandani na mwenzi wako. Ili kufanikisha kuwa na uwezo wa kuufanya muhogo kuwa mgumu kabisa mpaka ukawa mchungu(kudindish...

Fahamu Vyakula Vinavyotuua Kimyakimya Katika Mazingira Tunayoishi

Image
Tukumbuke kwamba uzima wa mtu unategemea sana kinga aliyonayo mwilini,kinga ambayo hujengwa na ulaji wa vyakula vyenye virutubisho vya aina mbalimbali. Kwa namna ambavyo Mungu ametuumba, mwili unapaswa kujilinda wenyewe dhidi ya maradhi ya kila aina. Ukiwa na kinga imara ya mwili siyo rahisi kuugua mara kwa mara. Magonjwa yanayojitokeza haraka pale kinga ya mwili inapokuwa chini, ni pamoja na kuugua malaria mara kwa mara, kifua kikuu, kutokwa na majipu, kutokwa uvimbe wa ajabuajabu katika mwili, kupatwa na mkanda wa jeshi, kupatwa na saratani na magonjwa mengine ya maambukizi. Je, Chanzo Cha Kushuka Kwa Kinga Mwilini Ni Nini? Ili uwe na kinga imara ya mwili, ni lazima uwe unakula mlo kamili unaojumuisha matunda, mboga za majani, nafaka na vyakula vingine vya asili, kwa sababu kila unachokula kina faida yake mwilini. Lakini siyo tu kula chochote kinachoitwa ‘chakula’, bali ule kilichosahihi. Katika maisha tunayoishi sasa, hasa mijini, idadi Kubwa ya watu hawali kabisa vyakula sahihi, ba...

Haya Ndio Mambo 7 Yanayosababisha Kutokwa Na Damu Katika Njia Ya Haja Kubwa (Rectal Bleeding)

Image
Hali ya kutokwa na damu katika njia ya haja kubwa mara nyingi hujionyesha yenyewe mara unapokuwa chooni baada ya kujipangusa na tishu (toilet paper), ama wakati kinyesi kinapotumbukia kwenye sink na kuyafanya maji kubadirika na kuwa mekundu. Wakati mwingine hali hii inaweza kujidhihirisha kwenye kinyesi baada ya kukiona kuwa na rangi nyekundu sana. Rangi ya damu inaweza kuonyesha mahali damu inakotokea: Damu nyekundu yenye kung’aa huonyesha damu inayovuka kwenye utumbo mpana au njia ya haja kubwa Damu yenye rangi ya weusi mara nyingi huvuja kutoka kwenye utumbo mwembamba au mpana Damu yenye rangi ya weusi ulioiva sana huvuja kutoka kwenye tumbo la chakula, kama vile kwenye vidonda vya tumbo Sio kwamba matatizo yote ya kuvuja kwa damu kwenye njia ya haja kubwa huonekana kwa macho. Wakati mwingine kutokwa na damu katika njia ya haja kubwa huonekana kwa kuangalia kinyesi kupitia darubini. Pia kuna vipimo vijulikanavyo ‘Hemoccult’ ambavyo hutumiwa na madaktari. Je, Dalili Zake Zinakuwaje? ...