Mambo 6 Yanayomfanya Mwanamke Kuhisi Maumivu Ya Tumbo Wakati Wa Hedhi Au Baada Ya Kutoka Hedhini
Wanawake wengi huhisi maumivu ya tumbo kabla au wanapokuwa hedhini. Lakini inaweza pia mwanamke akahisi maumivu ya tumbo anapokuwa hedhini. Maumivu haya mara nyingi huwa sio makali sana. Hata hivyo, ni muhimu kwamba unayafuatilia, hasa ikiwa kama yanakaa kwa muda mrefu. Maumivu ya tumbo wakati wa hedhi inaweza kuwa ni dalili ya magonjwa mbalimbali. Endelea kusoma Makala hii ujifunze dalili, visababishi, Pamoja na matibabu ya kukosa hedhi au kutokwa na damu ya hedhi nyingi kwa muda mrefu. Je, Nini Visababishi Vyake? Wakati mwingine maumivu ya tumbo baada ya hedhi huwa sio makali mno. Lakini kama una maumivu makali endelevu yanayodumu muda mrefu kuliko mzunguko wako wa hedhi, inaweza kuwa ishara kwamba una magonjwa kwenye tumbo lako la uzazi(uterus). Hapa nitakuelekeza visababishi vya maumivu ya tumbo unapotoka hedhini: 1. Endometriosis Endometriosis ni ugonjwa ambao hutoea pale seli zinazofanana na ukuta laini wa mji wa mimba(uterus) zinapoota nje ya mji wa mimba...